Diamond Ampa Shavu Dudu Baya Kwenye Wasafi Festival

Msanii mahiri wa muziki wa Bongo fleva nchini Diamond Platnumz amempa shavu Nono msanii mkongwe  wa Bongo fleva Dudubaya baada kumtaja kuwa miongoni mwa wasanii watakaotumbuiza kwenye taamasha la Wasafi Festival 2018.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Diamond ameweka wazi kuwa kuna wasanii wengi wakubwa ambao hawapati nafasi ya kutumbuiza kwenye matamasha makubwa kwa kisingizio kuwa hawajatoa nyimbo mpya.

download latest music    

Kaka yetu Dudu Baya muda mrefu watu hawajamuona kwenye show ya steji, sasa nawambia kwamba nitafurahi sana akiwepo kwenye show ya Wasafi Festival. Unajua sio tu Dudu Baya peke yake unajua kuna wasanii wengi wana sauti kubwa lakini sometimes hawapewi nafasi kwenye matamasha kwa sababu tu hawajatoa wimbo mwaka huu lakini kuna watu wanawapenda.

so wanaoandaa Wasafi Festival nitaongea nao na Dudu Baya pia wamuweke kwenye tamasha, nitafurahi kwa sababu nilikuwa tu namuonaga kipindi kabla sijatoka namuona anaimba”.

Dudu Baya au maarufu Kama Konki Konki Konki master amejizolea umaarufu Baada ya kendo yake inayoendelea kusambaa ya ushoga na bifu lake na Mange Kimambi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.