Dito Awatolea Povu Watu Wanaombeza Chid Benz

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka THT nyumba ya vipaji, Dito aliyetamba na wimbo wake wa ‘Wapo’ amewatolea povu Kali wale watu wote wanaomsema na kumbeza msanii wa rap ya Bongo fleva Chid Benz.

Wiki chache zilizopita Chid Benz alikamatwa kwa mara nyingine mjini Dodoma ambapo alikuwa amebeba madawa ya kulevya aina ya ‘heroin’. Hii siyo mara ya kwanza kwa chid Benz kuwekwa hatiani amekuwa akitumia madawa hayo kwa muda mrefu sasa.

download latest music    

Msanii Dito amewajia juu wale wote waliokuwa marafiki na washkaji wa Chid Benz ambao kwa sasa wanamsema vibaya na kumbeza msanii huyo kutokana na matatizo yake ya muda mrefu, Dito amedai sio vyema kumsema kwani hawatibu ugonjwa kwa kumsema.

Kwenye Interview aliyofanya na Enews ya East Africa TV Dito amewasihi watu wanaombeza Chid Benz waache tabia hiyo mara moja:

Kwanza haya ni matatizo yaayoweza kumkuta mtu  yoyote ni tatizo ambalo mtu yoyote anaweza akalipata yaani ukiteleza ukanguka inategemea ni utelezi gani kuna wengine wanahitaji msaada Mkubwa sana na ndio maana kuna siku nilisema sisi kama jamii tunakosea kushughulikia hili tatizo kwa sababu kwa upande mwingine tunakuwa tunazodoa, tunashambulia hawa waathirika wa madawa hatuwachukulii kama ni wagonjw lakini tungechukulia hivyo basi tungetafuta njia bora zaidi ya kuwapa tiba na wale watu wanaombeza hawamsaidii bali ndio wanamzidishia maumivu kwaiyo busara lazima itumike katika hili”.

Tangu Chid Benz ajiingize katika matumizi hayo ya madawa ya kulevya jitihada mbali mbali za kumsaidia zimefanywa na watu kadhaa bilamafanikio yoyotr mara ya mwisho Babu Tale alimpeleka Chid Benz sober house Bagamoyo lakini aliondoka baada ya muda mfupi kisha kurudia tena madawa ya kulevya.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.