Dokii Akanusha Kuhusika na Uongozi Mpya wa Mavoko.
Dada wa msanii Rich Mavoko, Dokii Wenslaus amefunguka na kukanusha taarifa za kuwa yeye ndio amehusika katika kumtafutia menejementi mpya na kwamba hakuna ukweli kuwa yeye ndio amempeleka katika lebel ya Billionares Kids.
Dokii alionekana akiwa bega kwa bega na rich mavoko kwa kipindi ambacho walikuwa wakishughulikia kesi yake na wasafi na ndie alietangaza kuwa rich mavoko alikuwa akinyonywa alipouwa akifanya kazi WCB.
Baada ya hapo walithibitisha kuwa msanii huyo kwa sasa amejisajili BASATA sio kama hapo awali alipokuwa akifanya kazi katika lebel hiyo bila kutambulika na serikali.
unajua watu wanaongea sana na wanaongea vitu ambavyo hawajui , wanaongea vitu vingi sana.Ungeenda kuuliza kwanza huko billionares kids ingawa uongozi haupo bado unalega lega hata wao watakanusha , hakuna kitu kama hiyo.