Dr. Cheni Baba Yangu Wa Sanaa- Lulu

Muigizaji wa Bongo movie Elizabeth Michael maarufu kama Lulu amefunguka na kuongelea uhusiano wake  na muigizaji mkongwe wa Bongo movie Dr. Cheni.

Kwa miaka mingi sasa Lulu ameonekana kuwa karibu sana na Dr. Cheni na sasa anafunguka na kuweka wazi kuwa ni mtu wa muhimu kwenye maisha yake.

download latest music    

Katika mahojiano aliyofanya na Kituo cha Times Fm, Lulu amefunguka na kusema kuwa watu wengi hawajui uhusiano Wake na Dr. Cheni Lakini yeye amemtaja kama baba yake katika Sanaa.

Watu wengi hawajui Lakini Dr. Cheni ni baba yangu wa Sanaa, tangu alipogundua kipaji changu Nikiwa na miaka mitano, amezidi kuwa mtu wa muhimu kwangu katika kuikuza na kuiendeleza Sanaa yangu”.

Lakini pia Dr. Cheni ameonekana na Lulu katika wakati ambao alikuwa anapitia kipindi kigumu ikiwemo wakati ambao aliwahi kupelekwa jela.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.