Elizabeth Michael “Lulu” afunguka kuhusu mipango yake ya ndoa

Staa wa sinema za Kibongo ambaye pia alikuwa msanii wa kwanza kuigiza akiwa umri mdogo Elizabeth Michael “Lulu”, na msanii ambaye amekuwa akikumbwa na skendo mbalimbali , kwa mara ya kwanza ameweka wazi kila kitu kwani mashabiki wake wengi wamekuwa wamekuwa wakiongea mengi kuhusu yeye kuolewa Katika mahojiano aliyoyafanya hivi karibuni Lulu aliweka wazi kuwa anashangazwa na watu wanavyomtabiria ndoa kila siku ikiwa yeye mwenyewe hajaweka wazi aliendelea kusema:

“Nafurahi kweli kusikia hizo habari, hivi mtu anawezaje kila siku anakutabiria ndoa? sasa nazungumza mwenyewe kama Lulu, hakuna kitu kama hicho, kwani ndoa anapanga Mungu kama ipo ipo tu”.

download latest music    

Pia Lulu aliweka wazi kuwa yeye kuishi maisha mazuri kwa kuvaa mavazi mazuri na kujiremba sio lazima kuwa na mwanaume mwenye pesa wa kumuwezesha kama watu wengi wanavyodhani  bali ni yeye mwenyewe kujishughulisha na shughuli zake nyingi anazofanya ambazo watu hawazioni.

kuna tetesi nyingi ambazo hutokea kwenye mitandao ya kijamii kuwa Lulu ni mjamzito, Lulu ameweka wazi kuwa anashangazwa na jinsi watu wanavyo mzushia kuwa ni mjamzito na ilhali yeye mwenyewe hajaweka wazi ila ni watu wachache wanaotunga habari hizo. Kwenye swala kuwa na familia hapo baadae Lulu alisema:

“Hakuna mtu ambaye hapendi kuwa na familia hasa watoto, lakini kwa sasa naona bado wangu haujafika siku ikifika endapo Mwenyezi Mungu atanijaalia basi ntafurahi kuwa mama”.

Lulu ambaye kwa sasa ni mmoja kati ya wasaanii wa Bongo movie anayefanya vizuri sana amekuwa kivutio kwa watu hasa kwa mavazi yake ya kupendeza na kuvutia huku wengi wamejikuta  wakikumkubali kama msanii anayevaa vizuri Bongo movie.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.