Esma Ashabikia Ndoa Ya Diamond na Tanasha

Dada wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Esma Platnumz ameibuka  na kuweka wazi mapenzi yake kwa wifi yake mpya Tanasha na kuweka wazi kuwa kama kaka’ke huyo atachukua uamuzi wa kumuoa kwake yeye anabariki kwa sababu ni chaguo lake.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Esma hadhani kama ni vyema kumchagulia kaka yake huyo mke, bali macho yake ndiyo yanaona wapi ni bora aangukie hapo na atakapopachagua na kumuonesha atampokea tu.

download latest music    

Unajua hata leo Diamond  akimtambulisha rasmi Tanasha kuwa anataka kumuoa, mimi kama dada, nitaona ni jambo la heri kwenye familia yetu ambayo kila kukicha tunamuombea apate mke bora”.

Diamond alianzisha mapenzi na binti huyo wa Kikenya Wiki chache  zilizopita  Lakini wamekwisha tangaza ndoa yao ambayo itafanyika mwezi wa pili mwakani.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.