Fahyma Adaiwa Kumsaliti Zari na Kujipendekeza Kwa Tanasha

Mzazi mwenzake na staa wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB Rayvanny, Fahyma amefungukia tetesi za uyuda  baada  ya kudaiwa kumsaliti Zari na kujiweka kwa Tanasha.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la  Risasi Jumamosi, Fahyma amesema kuwa anashangaa kwa nini watu wanamuita Yuda wakati hayupo hivyo na hajawahi kugombana na mtu yeyote aliyeachana na Diamond.

download latest music    

Hivi watu wakoje jamani sasa u-Yuda huo vipi? Kwa hiyo walitaka Diamond akibadilisha msichana mwingine basi huyu wa sasa mimi nisiwe na urafiki naye kwa sababu nilikuwa na urafiki na X wake?.

Hivi watu wana akili kweli? Mimi uhusiano wa Diamond unanihusu nini mimi? Sina mamlaka ya kumchagulia mchumba Diamond hata akimuacha Tanasha akawa na mwingine pia tukikutana kwenye sherehe nitaongea naye vizuri na kupiga naye picha kama kawaida kwa sababu mimi mwenyewe ni mpenzi mtazamaji tu.

Halafu kwanza huwa tunakutana kwenye event (hafla) tu, sijawahi kuwa na urafiki wa hivyo kama watu wanavyosema kwa hiyo waniache kabisa sitaki maneno jamani na mimi sio Yuda”.

Kama utakumbuka wakati Diamond yupo na Zari, Fahyma alionekana kuwa karibu na Zari na hata kuwepo pamoja katika mitoko mbali mbali walikuwa wote.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.