Ferooz: Biashara Ya Madini Ilinipoteza Kimziki

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva, Ferooz aliyetamba na vibao vyake ‘starehe’ na ‘boss’ amefunguka na kudai kitu kilichomfanya akae kimya mda mrefu kimziki ni kuingia kwenye biashara ya madini.

Baada ya kupotea kimuziki kwa zaidi ya miaka saba na kutajwa kama miongoni mwa wasanii waliofilisika na kufulia kabisa.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo cha televisheni cha East Africa, kupitia kipindi cha Enews Ferooz amefunfuka kuhusiana na biashara ya madini ilivyo mfilisi na uamuzi wake wa kurusi kwenye muziki mazima:

Biashara za madini kwa sasa nimeachana nazo sahivi nimeamua kurudi totaly kwenye mziki wangu , nilifanya fanya biashara ya madini lakini mwisho wa siku nikapoteza pesa zangu nyingi zikapotea ila sasa nimeamua tu kurudi kufanya music full package kama Ferooz nina kazi zangu mpya nimetoa mashabiki zangu wazipokee, nimeshatoa wimbo wangu mpya unaoitwa ‘nakaza roho’ kwa sasa nina timu yangu mpya ambayo tuna endeleza gemu”.

Pia kutokana na ujuzi alioupata kwenye biashara ya madini aliyofanya kwa miaka yote hii Ferooz kafunguka nini hasa ilikuwa sababu ya kupoteza pesa zote alizozipata kipindi anaimba madini:

Unajua kila biashara ina experience zake sasa mimi kwa kuwa nilikuwa nimeshazea kifanya muziki nikaingia tu bilakujua lolote na kuna vitu vingi sikuvijua nikaja kujikuta vitu vimeenda vibaya mwisho wa siku nikajikuta nimepoteza pesa nyingi basi mwishoni ndio nimeamua nirudi kwenye muziki 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.