Hamisa Amefunguka Kuhusu Bifu Lake na Lulu

Mwanamitindo na muigizaji wa Bongo movie, Hamisa Mobetto amemzungumzia muigizaji mwenzake Elizabeth ‘Lulu’ Michael aliyehukumiwa wiki iliyopita miaka miwili jela pamoja na uhusiano wao.

Siku za nyuma Hamisa na Lulu walikuwa na bifu kubwa tu ambalo lilitokana na wao kugombania mwanaume mmoja ambaye ni Majizzo. Hamisa alikuwa na uhusiano kwanza na Majizzo ambao ulipelekea kuzaa mtoto mmoja lakini baadae tena Majizzo aliachana na Hamisa na kuanzisha uhusiano na Lulu kitendo kilichopelekea mwanzo wa bifu la warembo hao wawili huku Hamisa akimtuhumu Lulu kwa kumuibia bwana ake hali iliyopelekea wawili hao kurushiana vijembe kwenye mitandao ya kijamii.

download latest music    

Baada ya Lulu kuhukumiwa Hamisa aliwashtua wengi baada ya kujishusha na kudai anamuonea huruma na hadi kufikia hatua ya kudai kuwa anampenda Lulu. Kitendo hiki kiliwaacha watu wengi midomo wazi na kwenye mahojiano na Millard Ayo alifunguka yafuatayo kuhusu uhusiano wake na Lulu:

Mimi kumposti Lulu ni kitu kidogo sana kwa sababu mwanangu Fantasy anapokuwa kwa baba yake Lulu naye anakuwepo ikimaanisha kuwa ni mama yake mdogo au mama wa kambo kwa mwanangu, lakini watu wanapenda tu kukuza mambo kwenye mitandao ya kijamii just because people don’t see each other doesn’t mean wana ugomvi mwisho wa siku mimi sina ugomvi na mtu na isitoshe nilivyo mposti Lulu ilikuwa ni kwa nia njema kabisa na kusema ukweli nimeumia Lulu kufungwa kwa sababu hata nilikuwa nikisafiri najua kabisa Fantasy nikimuacha na baba yake kunakuwa na mwanamke anamuangalia ambaye ni Lulu kwa sababu mimi siamini sana wafanyakazi wa ndani”.

Hamisa alifunguka hayo baada ya watu wengi kumuita mnafki baada ya kumuongelea vizuri Lulu lakini baadae alionekana kamualika kwenye sherehe yake Mama Kanumba ambaye anajulikana kama ni Hasimu Mkubwa wa Lulu.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.