Hamisa Amekuwa Akinivutia Sana , Hasa Alivyingia Katika Muziki :-Lulu Diva

mwanadada Lulu Diva amefunguka na kusema kuwa mwanadada Hamisa Mobeto ni moja ya wasichana anaowakubali na wamekuwa wakimvutia sana hasa maisha yake anayoishi lakini kukibwa zaidi amefurahi sana alivyojiingiza katika muziki.

Lulu diva anasema kuwa pamoja na kuwa mrembo na kuwa maarufu lakini ni mwanamke wa kipekee kwa sababu hakai kutegemea kitu chochote cha kupewa kutokwa kwa watu hasa wanaume kama ilivyo kwa wanawake wengine warembo.

download latest music    

Hamisa amekuwa akinivutia sana kwa sababu anajituma sana, ni msichana mrembo anaepigania kile anachokiitaji kila siku.unajua wanawake wengi wanafikiria kuwa ukishakuwa mzuri basi unakuwa unawezo wa kukipata chochote unachotaka kwa sababu tu unatumia uzuri wako lakini kwa hamisa ni tofauti sana pamoja na kuwa ni mama wa watoto wawili lakini amekuwa akijitahidi sana.—Alisema Lulu alipokuwa akiongea na Times Fm.

Ukiachana na upinzani mkubwa anaoupitia mwanadada Hamisa lakini amekuwa mwanamke jasiri na kupambana sana hata kama amekuwa na mapungufu yake mengi lakini anaweza kustahili sifa anazopewa na baadhi ya wasanii wenzake lama Lulu diva.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.