Hamisa Mobetto Amefunguka Haya Baada Ya Tetesi za Kuonekana na Diamond Dubai

Mwanamitindo na muigizaji wa Bongo movie Hamisa Mobetto kwa mara nyingine tena ameingia kwenye vichwa vya habari baada ya tetesi kuenea kuhusiana na uhusiano name baba mtoto wake Diamond.

Mwishoni mwa wiki iliyopita habari zilienea kwenye mitandao ya kijamii kuwa Diamond na Hamisa wameonekana pamoja nchini Dubai ambapo Diamond alikuwa anashiriki kwenye tamasha la One Africa Music Festival, huku sababu ya Hamisa kuenda Dubai ikiwa haijajulikana bado.

download latest music    

Picha mbali mbali zilisambaa mtandaoni zilizoashiria kuwa Diamond na Hamisa walikuwa katika eneo moja huku watu wakidai kuwa wamewaona pamoja kitendo ambacho kiliibua maswali Mengi kutokana na kuwa kiukweli Diamond yupo katika uhusiano na mama watoto wake na mpenzi wake Zari ambaye kwa sasa yupo nchini South Africa.

Mwishoni mwa wiki hii Hamisa alikuwa kwenye uzinduzi wa filamu yake inayojulikana kama ‘Zero player’ aliyocheza hivi karibuni katika mahojiano na Millard Ayo Tv alifunguka yafuatayo kuhusu tetesi hizo na uhusiano wake na mzazi mwenzie Diamond:

First of all kitu ambacho watu wanatakiwa wajue Mimi na Naseeb ni mtu na mzazi mwenzie yaani tumezaa mtoto sasa sijui kwanini watu wana-make a big deal wakisikia Hamisa kakutana na Diamond yaani hicho ni kitu ambacho watu wanatakiwa wazoee tu kwani ni baba wa mtoto wangu na mimi ni mama wa mtoto wake lakini hapana sikukutana na Naseeb Dubai watu sijui wamepata wapi hizo stori ama wamefikiria kitu gani ila kiukweli hata kama ningekutana naye ingekuwa kwa ajili yangu mimi na yeye kujua siyo watu wengine kujua”.

Pia Hamisa alifunguka na kudai kuwa yeye hana ugomvi wowote na familia ya Diamond hasa mama yake na Diamond kwani anamheshimu sana na pia anaamini mtu mzima hakosei lakini pia amedai anaelewa kama Zari anamchukia lakini yeye hana tatizo naye.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.