Harmonize Amtambua Mrisho Mpoto Kama Nembo ya Taifa.
Msanii Harmonize ameandika anachokifikiria kuhusu Mrisho Mpoto na kusema kuwa kwake yeye mrisho ni kama Nembo ya Taifa kutokana na mchango wake mkubwa alionao katika tasnia ya sanaa tangu anaanza muziki mpaka sasa.
Katika ukuasa wake wa instagram, Harmonize aliandika ujumbe mrefu ukiambatana na shukrani kwa kukbaliwa na Mrisho Mpoto akatika kufanya nae kazi ya pamoja .
binafisi nikiona sura yako naona kama inaashiria amani , upendo ,furaha, hekima nabusara , naamini tupo wengi sana wenye mtazamo kama wangu kuwa wewe ndio nembo ya taifa la tanzania kwani hata viongozi wetu pia wanajivunia sana uwepo wako katika sanaa, nichukue nafasi hii kusema asante sana kwa kuniamini na kunipa nafasi katika kazi yako. Mungu akubariki sana , hii ni kama ndoto kwangu.
Mrisho mpoto ni moja ya wasanii wakungwe na wakubwa sana nje na ndani ya afrika kutokana kna ukweli kwamba amekuwa moja ya tunu inayopita kutangaza utamaduni wa Tanzania kupitia nchgi nyingi sana na kazi yake imeonekana.