Hatimaye Ali Choki Arejea Stejini Baada Ya Kupona

Msanii mkongwe wa muziki wa Dansi nchini Ally Choki ametangaza kurudi mazoezini Baada ya Kuugua kwa miezi kadhaa.

Ali Choki ameanza mazoezi ya muziki katika bendi anayoifanyia kazi ya Super Kamanyola iliyopo jijini Mwanza.

download latest music    

Kwenye mazungumzo aliyofanya na gazeti la Ijumaa Wikienda, Ali Choki alisema alianza mazoezi rasmi wiki iliyopita ikiwa ni baada ya madaktari wake kumweleza kuwa kwa sasa amepona kwa asilimia 80 hivyo anamshukuru Mungu na Watanzania waliokuwa wakimwombea wakati akiwa hoi.

Tayari nimeshaanza rasmi mazoezi ya muziki ila kupanda jukwaani bado maana ninakula kwanza ugali wa kisukuma na sato nipate nguvu za kutosha na mwisho wa mwezi huu mambo yakiwa mazuri ndiyo nitaanza kupanda stejini kuwaburudisha mashabiki wangu“.

Ali Choki alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya presha na maradhi mengine yaliyopelekea kupumzika kufanya muziki kwa muda.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.