Hii Ndio ‘Michepuko’ Iliyomfanya Mpaka Diamond Akatoswa na Zari

Habari za Diamond na Zari kuachana bado zinatawala kwenye mitandao ya kijamii huku wengi wakiwa wameshtushwa kusikia kuwa couple iliyokuwa inapendwa na mashabiki zao imevinjika.

Huku sababu ya Zari kumwaga Diamond ikiwa ni wazi kabisa kuwa ni michepuko ambapo Zari ameweka wazi sababu juu iliyomfanya mpaka akafikia uamuzi wa kumuacha Baba watoto wake ni yeye kuzidisha kuchepuka.

download latest music    

Kwenye mahusiano yao yote kumekuwa na tetesi za Diamond kuwa na mahusiano na wanawake wengine ingawa mara nyingi amekuwa akikataa na kudai ni uzushi lakini pia na Zari amekuwa akimsamehe na wawili hao huishia kurudiana.

Baadhi ya michepuko ambayo inasemekana kuchangia kuvunja uhusiano wa Diamond na Zari ni hawa hapa:

1. Hamisa Mobetto 

Hamisa anatajwa kuharibu uhusiano wa Diamond na Zari tangu mwaka jana alipojitokeza na kukiri kuzaa naye kuanzia hapo mahusiano ya Diamond na Zari ikaanza kuyumba ingawa alimsamehe lakini bado kulikuwa kuna mpasuko tayari.

2. Irene / Officiallyn

Irene na Diamond wametajwa kuwa na mahusiano kwa muda mrefu sana tangu alipotokea kwenye video ya kwetu ya Rayvanny kama video queen kumekuwa na tetesi kuwa walikuwa wote South Africa at the same time akiwa na Zari na familia.

3. Shady

Huyu ni mwanamitindo kutoka nchini Rwanda tetesi za Diamond kutoka na Shady zilianza kusikika alitoa za kusafiri na kuelekea nchini Rwanda lakini zilipamba moto alipoenda Rwanda mwezi uliopita baada ya picha wakiwa pamoja kusambaa mtandaoni.

4. Mia

Mwezi uliopita kuna video ilisambaa mtandaoni ambayo ilimuonyesha Mia akiwa Madale ambapo baadae ilikuja kuonekana kuwa alienda pale na dancer wa Diamond ambaye alikuwa na mahusiano naye jambo ambalo Mia alikuja kulikana na kusema alienda pale na Diamond ambaye aliishia kulala naye.

5. Tunda

Uhusiano wa Tunda na Diamond ulikamata sana headlines ambapo inasemekana amekuwa mchepuko wake wa siku nyingi sana video iliyowaonyesha wakiwa pamoja ilisambaa mwezi uliopita tu.

6. Wema Sepetu

Wema na Diamond walitengeneza headlines wiki chache zilizopita baada ya kuonekana wakikumbatiana na kubusiana hadharani kwenye party huku kukiwa kuna tetesi kuwa wamerudiana.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.