Huddah Amchana Zari na Kamwambia Hana Ubosi Wowote

Socialite maarufu kabisa nchini Kenya, Huddah Monroe ameingia kwenye vita ya maneno mtandaoni tena na Zarinah Hassan ‘Zari’ ambaye ni mzazi mwenza wa msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Huddah amempanga Zari na kudai anajifanya Bosslady wakati hana lolote hii imetokana baada ya Zari kuweka video mtandaoni inayomuonyesha akionyesha simu zake tatu ambazo anatumia hivi sasa ambazo ni Samsung galaxy s8, Note 5 na IPhone X.

download latest music    

Baada ya kuonyesha simu hizo Zari alidai kuwa yeye ni tajiri na ndio maana amenunua simu zote kali kwa wakati huu huku akionyesha saa yake aliyodai ni Rolex. Baada ya video hiyo kusambaa mtandaoni Huddah alimjibu kuwa yeye amekuwa anatumia IPhone X tangu ilivyotoka mwaka jana hivyo yeye ndio Boss.

Kupitia ukurasa wake wa SnapChat Huddah aliandika maneno yafuatayo:

Funny how people buy iPhone X after it came out long ago and social media can’t sleep…some of us have been using iPhone Z from the day it came out and we don’t flaunt small things like that because we’re used to it! Act like a boss! Tumia pesa ikuzoee”.

Zari na Huddah ni maadui wakubwa na sio mara ya kwanza kwa wawili hawa kurushiana maneno mtandaoni wamekuwa wakitofautiana mara kwa mara lakini ustajaabu kujua kuwa mara ya kwanza walikuwa marafiki wakubwa.

Zari na Huddah Enzi za Urafiki wao.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.