Jibu la Ali Kiba Baada Ya Kualikwa na Diamond Lazua Utata

Siku mbili  zilizopita Staa wa Bongo fleva na mkurugenzi wa WCB Diamond Platnumz alimualika hasimu wake Ali Kiba kuperfom kwenye tamasha la Wasafi Festival litakaloanza siku za karibuni.

Lakini Ali Kiba amedaiwa kumjibu Diamond kimagumashi kwa kupost picha ya mchekeshaji maarufu duniani, Mr. Bean na kuandika maneno kadhaa.

download latest music    

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Kiba amepost picha hiyo yenye maneno; ‘Thank you for listening, To my presentation’, halafu chini ya post hiyo akaandika “Your welcome”.

Mashabiki wengi walianza kuzungumza mitandaoni na kusema siyo rahisi kwa Alikiba kukubali kuungana na Diamond kwenye Wasafi Festival huku wengine wakisema Alikiba akubali tu, na hadi kufikia wengine kusema Alikiba atatoa jibu lake baya au la kizarau sana.

Mange pita aliweka wazi kuwa Ali Kiba hawezi kukubali kuperfom na Diamond kwani kwa kufanya hivyo itakuwa anajimaliza yeye kwani Bifu lake na Diamond likiisha tu basi na ndio mafanikio yake mwisho kwani anabebwa sana na Bifu na Diamond.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.