Joh Makini Adai Haoni Tatizo Kwa Wasanii Wa Kiume Kuvaa Vikuku

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayetamba kwa staili ya kuchana kutoka katika kundi la Weusi Joh Makini au Mwamba wa kaskazini amedai haoni tatizo kwa wasanii wa kiume kuvaa vikuku kama wanataka kufanya hivyo.

Joh Makini wameweka wazi kuwa wasanii wa kiume kuvaa vikuku miguuni sio kitu cha ajabu kama watu wengi wanavyodhani kwani anaamini ni fasheni kama fasheni nyingine.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Bongo 5, amesema kuwa wasanii ni watu ambao wanaishi na fasheni na style mbalimbali hivyo msanii kuvaa kikuku ni maamuzi yake na yeye anachukulia kawaida kabisa suala hilo;

Sijui kesho lakini mimi nachukulia kama style yake kama mimi nilivyoamua kuweka Rasta kuna wengine wameamua kuvaa vikuku wengine kutoboa pia na masikio lakini Sioni tatizo lolote kama mtu ameamua kuchagua aina ya maisha anayoishi”.

Wiki iliyopita msanii  wa muziki Diamond Platnumz aliposti picha kwenye ukurasa wake wa Instagram akionekana mguuni akiwa amevalia cheni maarufu kwa jina la kikuku jambo ambalo lilisababisha ashambuliwe na mashabiki wake mitandaoni.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.