Juhudi za Madee Katika Kumuandaa Mtoto Wake Kimuziki.
Msanii wa muziki wa bongo fleva Madee amekuwa mstari wa mbele katika kumuandaa mtoto wake mdogo wa kike kuwa msanii wa baadae huku akifuata nyayo za baba yake ili kufikia hatua aliyoifikia yeye.
Katika ukurasa wake wa instagram, madee ameweka pich aya mtoto wake huyo wa kike akiwa studio akitaka kuikaribia mic na chini ya picha hiyo madee aliandika”ipo siku utaifikia mwanangu wala huna haja ya kuharakisha”
Maneno hayo yanaonyesha ni jinsi gani Madee ameshatambua kipaji cha mwanae na amekuwa akifurahi kumuona mtoto huyo akiwa na kipaji kama chake na amekuwa akitamani sana mtoto huyo kufikia alipofikia yeye.