Kajala Awatolea Povu Wanaohoji Umri Wa Mtoto Wake

Muigizaji  wa filamu za Bongo Movie Mrembo Kajala Masanja amewatolea povu zito watu wote ambao wamekuwa mstari wa mbele kuhoji umri wa binti yake Paula.

Wiki iliyopita Kajala aliposti picha kadhaa Kwenye mitandao ya kijamii kwa ajili ya kusherekea birthday ya binti yake Paula lakini utata ulikuja baada ya mashabiki kuhoji umri wa mtoto huyo huku wengi wakikataa kuwa ana miaka 16.

download latest music    

Watu wengi walimjia juu Kajala wakimtuhumu kwa kumpunguzia umri binti yake na kudai anaonekana mkubwa kuliko miaka 16 na kudaiwa kupunguza miaka ya mtoto ili na yeye aonekane kama ana umri mdogo.

Kwenye mahojiano na gazeti la Amani hivi karibuni mara baada ya kumposti mwanaye huyo kwenye ukurasa wake wa Instagram na kumpongeza kufikisha miaka 16, Kajala alisema ameshangazwa na watu walioanza kumsema mwanaye kuwa ana zaidi ya miaka 16.

Mimi naona kubishana na watu wa Insta ni kujisumbua kwa sababu mtoto nimemzaa mwenyewe lakini wanaibuka watu wanajifanya wanajua umri wake kuliko mimi, basi waendelee kuamini ni mkubwa zaidi”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.