Kala Jeremiah Ameongea Haya Baada ya Kumwagiwa Sifa Kibao na Makamu Wa Rais

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayetumia miondoko ya kuchana hip hop, Kala Jeremiah amesema kuwa alipokea kwa mshtuko taarifa za kusifiwa na makamu wa raisi.

Wiki iliyopita Makamu wa Raisi Mama Samia Suluhu Hassan alimsifia Kala Jeremiah kwa nyimbo yake mpya inayoitwa ‘kijana’. Mama Samia alifunguka hayo kwenye kikao cha CCM kilichofanyika Dodoma ambapo alikuwa anawaasa wasanii wa Bongo fleva kuimba nyimbo za kuhamasisha na kufundisha jamii.

download latest music    

Ambapo kwenye hotuba yake hiyo alidai kuwa ni vyema wanavyotoa nyimbo kama ‘Natamba; ya Aslay na watu wanazipenda lakini umefika wakati wasanii watunge nyimbo kama ya Kala Jeremiah ‘kijana’ ambayo inawaasa vijana wenzake kufanya kazi kwa bidii na juhudi zote ili tu waweze kujenga taifa.

Baada ya kumwagiwa sifa hizo mbele ya waandishi wa habari wote Kala amefunguka haya ili kuelezea ni jinsi gani alijisikia na anachukulaje heshima hiyo aliyopata kutoka kwa kiongozi mkubwa serikalini;

Nilipigiwa simu na watu mbali mbali kuwa nimepata pongezi kutoka kwa makamu wa raisi kwangu mimi ilikuwa ni mshtuko mkubwa sana na ni kitu kikubwa sana kwa msanii yoyote yule kutamkwa hadharani ilikuwa ni heshima kubwa sana kwangu na imenifanya nione kuwa nina deni kubwa sana la kuendelea kupigana kwenye kuendelea kuiongelea jamii na kuendelea kuwaongelea wale  watu ambao hawana sauti na imenipa nguvu ya kuendelea kufanya kile ninachoendelea kufanya”.

Kala ni moja kati ya wasanii wachache nchini aliyejipatia umaarufu kwa kuimba nyimbo za siasa na nyimbo ambazo zinagusa matatzo ya kijamii tofauti na wasanii wengine ambao huimba mapenzi na vitu vingine vya tofauti.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.