Kala Jeremiah na Ndoto Ya Kujenga Shule Kwa Ajili Ya Yatima na Watoto wa Mitaani

Msanii wa muziki wa hip hop nchini Kala Jeremiah ameibuka na kuweka wazi mipango yake ya kujenga shule ambayo itawasaidia Watoto yatima na Watoto wa mitaani.

Kala amefunguka na kusema kwa muda mrefu imekuwa ni ndoto yake kufanya kitu kikubwa kama hicho ili aweze kuwasaidia Watoto wanaoishi katika mazingira magumu na wasiojiweza.

download latest music    

Kwenye mahojiano yake aliyofanya na Millard Ayo, Kala Jeremiah ameongea haya kuhusu mpango Wake huo kabambe:

Nina Ndoto ya kujenga shule kubwa ambayo watasoma watoto yatima bure, itakuwa boarding school kubwa sana ambayo pia itahudumia watoto wote wanaoishi katika mazingira magumu na nikitimiza ndoto yangu hiyo hata Mungu akinichukua baada ya hapo nadhani nitakuwa nashangilia”.

Kala Jeremiah amekuwa mmoja kati ya wale wasanii ambao wamekuwa wakifanya muziki wa kuleta tija ambao unajikita katika kugusa mambo muhimu katika jamii.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.