Kauli ya Elizabeth ‘Lulu’ Michael kuhusu upendeleo na uchawi

Elizabeth Michael ametoa ujumbe maalum kwa mashabiki wake kuhusu mapendeleo na uchawi. Staa huyo wa filamu ya Bongo alitoa mawaidha yake kwa kusema kuwa kibali ndo huwezesha mtu kunawiri kwa anachofanya wala sio mapendeleo ama uchawi kama baadhi ya watu wanavyoamini.

Soma ujumbe alioandika Elizabeth hapo chini:

download latest music    

Umeshawahi kukutana na watu wa aina hii;

1.SHULENI; Mwanafunzi nayependwa sana Na waalimu na staffs wa shule…anaaminiwa zaidi Hata kwenye baadhi ya mambo muhimu ya kishule…Ila kwa wenzake anaonekana kama hastahili na anapendelewa.

2.KAZINI; Mfanyakazi anayependwa na kuaminiwa zaidi na boss na aina ya watu flani wakubwa katika ofisi/taasisi/kampuni…Huyu inawezakana sio bora kuliko wengine pengine ni mwenye kiwango cha chini kabisa lakini anasikilizwa na kushiriki kwenye mambo makubwa au yupo kwenye nafasi kubwa kuliko wanao onekana wanastahili.

Huyu sasa anaonekanaga mchawi tuna atahusishwa na mahusiano na story nyiiingii feki.

3.FAMILIA; Mtu anayeaminiwa sana Na familia na hakuna majadiliano au maamuzi yoyote yatafanywa na familia bila uwepo wake…Huyu kama amebarikiwa uwezo wanafamilia wengine watasema anapewa hiyo nafasi kwasababu ya uwezo wake kama Ana maisha ya kawaida ataonekana anapendelewa.

4.MAHUSIANO; Mke/Mume/Mchumba anayeonekana hafai kwa mwenza wake…Labda ki muonekano,umri,uwezo,historia au chochote tu lkn muhusika ndo anamuamini na kumpenda…Huyu sasa anaonekana mwanga maana kwenye uchawi tunaonaga amevuka

Hizo ni baadhi tu ya jinsi watu wengi tunavyoona vitu katika makundi hayo….Ila ki KIUHALISI na KIROHO hakuna upendeleo wala uchawi bali kuna kitu kinaitwa KIBALI(Kwa wakristo watanielewa zaidi)

Mtu yoyote aliyepewa KIBALI NA MUNGU anaoneka kama mtu anayependelewa katika mambo mengi au mtu anayetumia nguvu ya ziada kufanikisha mambo yake…ni kwasababu ukiwa na KIBALI unauwezo wa kuingia/kutoka mahali pagumu kuingilika/kutoka kwa uwezo wa ki binadamu,unaweza kukaa/kushirikiana na watu wakuubwa ambao kwa uwezo wako binafsi usingeweza kukaa/kushirikiana nao,una uwezo wa kuwa katika nafasi ambazo unaonekana hustahili kuwepo….Yaani kiufupi ukiwa na KIBALI UNAWEZESHWA KUYAWEZA YASIYOWEZEKANA katika hali ya kawaida

Nashukuru MUNGU kwa kuwa mmoja kati ya wengi waliopata KIBALI chake…Mambo mengi yaliyopita,yaliyopo na yanayoendelea kutokea kwenye maisha yangu yanathibitisha KIBALI chake.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere