Kim Nana Awataka Wadangaji Wajaribu Ujasiriamali

Video vixen anayefanya vyema sasa Kwenye ulimwengu wa muziki wa Bongo fleva Lilian Kessy maarufu kama Kim Nana amewataka wanawake wadangaji kutafuta biashara ya kufanya.

Kim Nana amefunguka na kudai anawashangaa sana wanawake wanaofanga mjini badala ya kutumia muda wao na nguvu zao kwa ajili ya kutafuta biashara za kufanya.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Risasi Jumamosi, Kim Nana amesema kuwa anawashangaa wasichana wengi hasa mastaa wanaodanga wakati fursa za biashara zipo nyingi na mbali na biashara kazi za kufanya zinapatikana.

Unajua sisi ambao tuna majina tayari yawe makubwa au madogo ukijaribu kitu kushindwa ni ngumu sana hivyo mimi nawashauri wanaodanga wabuni hata miradi au wajitokeze kwenye makundi yanayofunza ujasiriamali watatoka tu kimaisha“.

Kim Nana pia amewataka watu kufuta dhana inayosambaa kuwa mavideo Queen wote ni wadangaji kutokana na kipato chao kidogo wanachopata kutokana na kazi hiyo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.