Kumbe Ruby Hakuwa Na Mimba

Miezi kadhaa ya nyuma kulikuwa na habari karibia kila kona zikiongelea habari ya msanii wa kike aliyekuwa akitambaa sana katika muziki wa Bongo Fleva  Hellen George kuwa ni mjamzito lakini kumbe habari zile hazikuwa za kweli, tetesi izo ambazo zilikaa kwa muda kidogo mitandaoni mpaka aliyempa ujauzito kujulikana kuwa ni kijana mmoja kutoka Arusha zimekanushwa na Ruby mweneyewe na kusema kuwa habari za yeye kuwa ni mimba ni uongo ilikuwa ni mimba feki.

Hata hivyo tetesi izo zimekuja baada ya yeye mwenyewe kuweka picha yake katiaka mitandao  akionyesha tumbo lake kuwa kubwa ivyo kama kawaida ya mitandao na mihemko ya mishabikaia walianza kuongea kuhusu kuwepo kwa ujauzito huo, hata hivyo Ruby mwenyewe hakutaka kubisha kuhusu maneno ya mashabiki akaendelea kuwapa moyo kuwa kweli yeye ni mjamzito kweli.

download latest music    

Akiongea katika mahojiano  na gazeti moja nchini Ruby ameamua kuelezea ukweli kuhusu ukweli wa mimba hiyo.Ruby anasema kuwa ni kweli alipost picha ya tumbo kubwa katika mtandao lakini siku iyo alikuwa ametoka kula pilau kwa mama yake aliloandaliwa na mama yake huyo , hata hivYo baada ya yeye kushiba akaamua kutunisha tumbo kama utani na kupost katika mtandao wake Instagram , picha ambayo ilifanya mashabiki  waweke maamuzi  ya moja kwa moja kuwa Ruby  ni mjamzito.

“Kwa kuwa  watu walinianzishia hilo na mimi nikawa ninaitikia kuwa ni kweli lakini sikuwa na mimba  ingawa hata nilipoulizwa na baaadhi ya watu nilijibu kuwa ni kweli nina mimba  na nilimtaja mpaka baba wa watoto wangu ambae alihusika na mimba hiyo  na kumuonesha katika mitandao  lakini kwa sasa sitaki kumzungumzia kabisa’ alisema Ruby.

Msanii huyo wa kike aliyekuwa akilelewa kumuziki kutoka jumba la muziki la THT , kwa sasa yupo kimya kutokana na yeye kutokuwana maelewano mazuri na menejimenti yake , lakini alipokuwa akifanya mahojiano katika vyombo mbalimbali vya habari Ruby alisema kuwa kwa sasa anajiandaa vvyema na yupo karibu kurudi katika muziki hivyo mashabiki wake wakaae wakimsubiri kwa nyimbo nyingi nzuri.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.