Lady Jay Dee: Mimi ni Shabiki Mkubwa wa Aslay

Malkia wa muziki wa Bongo Fleva nchini Lady jay dee ambaye ni mkongwe wa mziki huo tangu miaka ya 90 ambaye pia anaweza kuwa mmoja kati ya wasanii bora wa kike Afrika Mashariki nzima kutokana na ukongwe wake na kutochuja kwenye fani na kuweza stahimili kukaa kwenye chati kwa miaka yote hiyo.

Mwanamuziki huyo amekiri kipaji cha Aslay na kusema  kuwa anamkubali, Aslay ni msanii anayekuja kwa kasi ya ajabu sana katika mziki huu wa Bongo fleva. Aslay ambaye amejitoa katika kikundi cha Yamoto Band hivi karibuni amekuwa akitoa nyimbo nzuri kutokana na staili yake hiyo ya kuimba nyimbo zake kwa hisia kali. Aslay tangu ameanza kufanya muziki kama Solo Artist ameweza kufikisha views milioni kumi katika chaneli yake ya Youtube.

download latest music    

Lady Jay Dee alieleza haya alipokuwa katika kipindi cha THE PLAYLIST wakati ambapo alitakiwa kuchagua nyimbo tano anazozipenda ambapo mojawapo ilikuwa nyimbo ya Aslay “Muhudumu” na kufunguka kuwa  yeye ni shabiki mkubwa wa msanii huyo na muziki wake na kwasababu ana melodies za kipekee na nzuri sana kwenye nyimbo zake.

Lady Jay Dee ametoa nyimbo yake mpya inayoitwa “I miss you” inayofanya vizuri redioni na pia Aslay naye ana nyimbo kadhaa zinazofanya vizuri alipoulizwa kuwa endapo watashirikiana kufanya kazi mbeleni alijibu kuwa atafurahi ikiwa hivyo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.