Lulu Diva Amkana Ney Wa Mitego Hadharani.

Ni zaidi ya mwaka saa tangu kuwepo kwa habari kuwa msanii wa kike Lulu Diva kuwa na mahusiano na msanii anaefanya vizuri katika kazi zake za muziki Ney Wa Mitego, mwanadada huyo akanusha tuhuma hizo na kukutaa kata kata huku akisema kuwa Ney hana sifa za kuwa mpenzi wake.katika kipindi cha nyuma wawili hao walikuwa wakionekana pamoja na hata kuna baadhi ya mahojiano waliyokuwa awakifanya walikiri kuwa pamoja lakini cha ajabu ni kwamba kwa sasa mwanadada huyo amekataa kata kata kuwa yeye hana mahusiano na Ney Wa Mitego.

Hata hivyo Lulu Diva ameamua kutoa povu ili na kulielekeza kwa Ney Wa Mitego na kusahahu kuwa alishawahi kukiri kuwepo kwa uhusiano wao.’Ney hawezi kuwa type yangu hata siku moja,na hajawahi na hawezi kuja kuwahi  hata siku moja niwe na Ney” aliongea Lulu Diva

download latest music    

Hata hivyo Lulu aongezea kwa kusema kuwa Ney Wa Mitego hajawahi kumvutia kabisa katika swala zima la mapenzi.”kwanza hajawahi kunivutia, na kamwe hawezi kunivutia, hivi mimi kweli niwe na Ney, haiwezekani kabisa  kwa mwanaume kama yule” aliendelea kusema. Msanii huyo  wa kike ambae kwa hivi sasa na yeye ameamua kujishughukisha na shughuli za muziki kwa kuimba ilhali kipindi cha mwanza alikuwa ni video queen wa baadhi ya nyimbo za wasanii wenzie lakini pia ametokea katika baadhi ya tamthilia mbalimbali katika vituo vya televisheni.Amekuwa  akifanya vizuri katika kazi zake za muziki na  kutoa nyimbo kama ‘Usimwache’,’Utamu’ na ‘Give to me’ .

Ikiwa ni muda sasa umepita tangu wawili hao wafanye interview ikimuonyesha Lulu Diva akiwa na Ney Wa Mitego huku wakikiri kuwa walishawahi kuwa wapenzi lakini kwa sasa ni marafiki na kukiri wanaweza kufanya kazi pamoja kwa sasa muda wa mapenzi ulishakwisha na wakiamua kufanya serious basi wataweza kufanya muziki, inakuwa ni hali ya kushangaza kwa Lulu Diva kukataa kuwepo kwa mahusiano  baina ya wawili hao. hata hivo inawezekan akukawepo kwa marumbano baina ya wawili hao inayopelekea kuwepo kwa maneno hayo.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.