Mama Mobetto Atoa Masharti Mazito Kwa Mkwe Wake

Mama mzazi wa Msanii wa Bongo fleva na mwanamitindo Hamisa Mobetto, Shufaa Rutiginga maarufu kama Mama Mobetto ameibuka na kutoa masharti kwa Mpenzi wa mwanaye.

Mama Mobetto amefunguka hayo Baada ya picha kusambaa kwenye mitandaoni ya kijamii zilizomuonyesha Hamisa na Mpenzi Wake Josh Adeyeye nchini Marekani.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Mama Mobetto alipoulizwa kuhusu picha hizo alisema, msimamo wake ni kwamba, hata kama picha hizo zinaonekana na yeye kuziona kwenye mitandao lakini bado anamtambua tu kama hawara.

Mama Mobeto alisema, kama kweli jamaa huyo anamhitaji mwanaye basi masharti anayompa ni kufika nyumbani kwanza nyumbani kwake kujitambulisha ili amjue vizuri yeye pamoja na ndugu zake.

Hivi jamani umeona wapi mzazi ambaye anajua maadili amuongelee hawara wa mtoto wake ambaye hajatambulika rasmi? Aje nyumbani, ajitambulishe, hapo sasa nitakuwa free kumuongelea, lakini habari za kwenye mitandao siwezi kuzizungumzia”.

Mobetto alimuanika Mpenzi Wake huyo siku chache zilizopita baada ya kuisha kwa mahusiano na aliyekuwa Mpenzi na baba mtoto Wake Diamond Platnumz.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.