Mama Mobetto: Nitamsapoti Mwanangu Kwa Kila Jambo

Mama mzazi wa Mwanamitindo Hamisa Mobetto, Shufaa Rutaginga maarufu kama Mama Mobetto amefunguka na kuapa kuwa upande wa mwanaye na kumsapoti katika mambo anayopitia.

Mama Mobetto amedai hata kama watu watamtenga mtoto wake yeye atakuwa katka upande wake na kumsapoti kwa kila jambo kwani anajua uchungu wake kama mama.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Ijumaa Wikienda, Mama Mobetto amefunguka kuwa, watu wakiendelea kumzushia mwanaye mabaya na kumsema kila kukicha kazi yake yeye siku zote ni kumpa moyo na kumsihi asikate tamaa.

Kazi yangu kubwa kwa mtoto wangu ni kumpa moyo na kumuonesha ni jinsi gani ninampenda maana naamini ni changamoto tu anapitia, lakini zitaisha na zitamfanya kusimama imara”.

Hamisa amekuwa akipata wakati mgumu Kwenye mitandao ya kijamii tangu azae na Diamond kwani Familia ya Diamond imekuwa ikiweka wazi kumchukia lakini pia mashabiki wa Zari wamekuwa wakimpa kipindi kigumu.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.