Masanja Atetea Kitendo Cha Diamond Kuvaa Kikuku na Kudai Mungu Anaruhusu Kwenda na Fasheni

Mchekeshaji maarufu Masanja Mkandamizaji ambaye sasa amegeukia Injili na kujiita Mchungaji amefunguka na kumkingia kifua Diamond Platnumz kwa kitendo chake cha kuvaa kikuku.

Masanja amefunguka Kwenye mahojiano na Masanja Tv, na kudai kuwa kwa imani yake ya Kikristo kuvaa kikuku mguuni kwa mwanaume sio dhambi kwani inahesabiwa kama cheni yoyote unayoweza kuvaa na Mungu hajakateza watu kwenda na fasheni.

download latest music    

Kama mchungaji nasema mwanaume kuvaa kikuu mguuni sio dhambi, lakini nikawaambia kwenye maadili kuvaa kikuku unamaanisha nini? soo shinda ikiwepo kwenye maadili haina maana ni dhambi watu wanadhani kuwa vitu wasivyovipenda wao kuviona, vitu ambavyo sio maadili mazuri wanafikiri kuwa ni dhambi kuna tofauti sana juu ya hivyo vitu. Kwa hiyo narudia tena kusema mwanaume kuvaa kikuku katika Biblia sio dhambi”.

Lakini pia Masanja amesema Cheni ni cheni tu na hakuna mtu wa kumpangia binadamu mwenzie sehemu ya kuvaa na hakuna cheni ya mwanamke zote ni cheni tu.

Kikuku ni cheni tu, hakuna cheni ya kivulana wala cheni ya kike cheni ni cheni na ukiamua kuvaa mkononi au shingoni sio dhambi kufikiria vibaya mtu kuvaa cheni mguuni huo ni uchizi wa hali ya juu. Kwahiyo kama kuna mtu anaona kuvaa micheni miguuni ndio raha muacheni avae”.

Pia Masanja amesema kuwa Mungu hajamuumba binadamu aokoke ili awe nyuma ya fasheni bali alimuumba aendane na fasheni.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.