Mbasha Apangua Tetesi Za Kupombeka na Wolper

Msanii wa nyimbo za injili nchini Emmanuel Mbasha ameibuka na kupanguia tetesi zote zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii ya kwamba mtumishi huyo wa Mungu alikuwa amekaa na msanii wa Bongo movie Jacqueline Wolper wakinywa pombe.

download latest music    

Kwenye interview aliyofanya na kituo kimoja habari, Mbasha amekanusha tetesi hizo na kudai kuwa alikuwa anakunywa soda. Mbasha amesema watu wamemjia juu kwa kukaa karibu na Wolper na kusema akiendelea kukaa karibu na  Wolper atampoteza na pengine anaweza akafanya mambo ambayo hayaendani na wokovu wake kama watu walivyomzoea kwamba yeye ni mtu wa dini.

Mimi na Wolper ni marafiki wa karibu na ukweli ni kwamba mimi nampenda Wolper kama dada yangu na namkubali kwa kazi zake anazozifanya hata hivyo naamini kwamba na yeye ananipenda kwa kuwa tumekuwa karibu kwa muda mrefu sasa”.

Lakini pia Mbasha alimalizia huku akitolea maelezo picha ambazo zimesambaa mitandano zikimuonyesha akiwa karibu na Wolper na kusema kwamba picha hizo zilitokana na kazi ambayo waliipata kwa pamoja ikawakutanisha na kuwaweka karibu.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.