Mboso Atangaza Ndoto Yake ya Kumnunulia Diamond Nyumba ya Kifahari

Msanii kutoka kundi la WCb mbosso amefunguka na kusema  kutokana na mafanikio yake anayoyapata kutoka WCB anaona kuwa hana kitu cha kumlipa bosi wake diamond platinumz kwa sasa anaona aliyofanyiwa ni makubwa kuliko anachoweza kukitoa yeye.

Mbosso anasema kuwa ,  amekuwa akiwaza kila siku kitu cha kumpa lakini hakioni lakini ndoto yake kubwa ni kumnunua bosi wake nyumba kubwa au gari la kifahari kama zawadi ambayo pia anajua haitatosha kuonyesha shukrini zake zaidi ya sala .

download latest music    

Mbosso anasema kuwa kila mmoja yuko na njia yake ya kusema shukrani, kama harmonize aliamua kuchora tatoo isiyofutika kama shukrani ya uwepo wake na umuhimu katika maisha yake lakini yeye anaona bado kuna kitu kikubwa anaweza kufanya ingawa kwa sasa amekuwa akimuombea kila kukicha.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.