Mc Pilipili Amtaka Ben Pol Amuoe Mpenzi Wake Mpya
Mshehereshaji maarufu Emmanuel Mathias maarufu kama Mc Pilipili ameibuka na kumpa ushauri staa wa Bongo fleva Ben Pol wa kumtaka amuoe Mpenzi Wake Mpya.
Wiki chache zilizopita Ben Pol alianika mapenzi yake hadharani na binti wa Kikenya anayeitwa Anerlisa Mugai ambaye anatajwa kuwa mtoto wa kigogo na pia binti anayeogelea kwenye pesa.
Mc Pilipili ameibuka na kutia neno kwenye mahusiano ya Ben Pol na Anerlisa ambapo amesema watu wa kabila lake siku zote huwa wanapenda kweli kweli, hivyo akamtaka Ben Pol kuchukua maamuzi ya kuoa.
Wagogo tukipenda hua tunapotelea kabisa Ben Pol nakuelewa kaka yangu huu mwaka wetu kama tulivyoongea kaka”.
Mc Pilipili amekuwa kwenye headlines kwa siku mbili hizi Baada ya video yake alipokuwa anamvisha pete Mpenzi Wake na kuangua kilio kusambaa kwenye Mitandao ya kijamii.