“Mh. Temba Alimfumania Mke Wake, Walishaachana” – Bi. Cheka

Msanii wa Bongo fleva aliyetamba miaka ya nyuma na nyimbo zake kama ‘Ni wewe’ ‘Naenda kusema kwa mama’ na nyinginezo nyingi Bi. Cheka aliyehipatia umaarufu baada ya kuwa msanii mzee kuliko wote amerudi upya kwenye headlines.

Bi. Cheka amerudi upya hivi karibuni baada ya kumrushia tuhuma nzito msanii mkongwe Mh. Temba akidai kuwa yeye na mke wake wameachana baada ya kumfumania mke wake na njemba nyingine.

download latest music    

Chanzo cha ugomvi huu kilianza baada ya Bi. Cheka kudai kuwa kutokana na kuwa na umri mkubwa ameumwa mpaka kukaribia kufa lakini amesikitishwa hakuna hata msanii mwenzake aliyeenda kumuona huku akimrushia tuhuma Mh. Temba aliyeshirikiana naye kwenye wimbo wake wa ‘Ni wewe’ na pia Mkubwa Fela aliyekuwa meneja wake.

Baada ya kumrushia tuhuma hizo Mh. Temba aliibuka na kusema kuwa hawezi kufikia maanani sana anachokisema Bi. Cheka kwa sababu ni mzee hivyo sio kosa lake.

Baada ya kusikia jibu hilo Bi. Cheka hakupendezwa alimwaga povu zito Kwenye mahojiano aliyofanya na Enews ya East Africa Tv ambapo alifunguka haya mazito kuhusu Mh. Temba na mkewe:

Kwanza huyo Mh. Temba mbona hasemi kuwa mke wake kapata bwana mwingine aseme ukweli hapa alimfumania ndani ya nyumba yake mwenyewe akiwa na mwanaume mwingine ya kwake mazito kuliko ya kwangu mbona yake siyaingilii wala sina habari nayo”.

Bi. Cheka aliongea kwa uchungu akidai amekerwa na usaliti aliofanyiwa kwani alitegemea Temba na TMK watamkubuka akiugua kama ilivyokuwa zamani wakati marafiki.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.