Miriam Odemba- Nimekumbuka Sana Nyumbani

Mlimbwende mkongwe Bongo Miriam Odemba ambaye kwa miaka mingi amekuwa akiishi nchini Ufaransa amefunguka na kukiri kuwa amekumbuka sana nyumbani.

Miriam Odemba ametoa la moyoni kuwa akili yake kwa sasa amekuwa akiwaza nyumbani Tanzania hivyo kukosa raha.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Miriam Odemba alisema kuwa hata mtu akae nchi za watu kwa miaka mingi, lakini bado picha ya nyumbani haifutiki akilini.

Siyo kwamba hakuna maisha mazuri au sipati ninachotaka, lakini siku zote nyumbani kuna ladha yake. Nimekumbuka sana nyumbani na kungekuwa karibu kwa kweli kila wakati wangeniona”.

Pamoja na kuishi mbali na Tanzania, Lakini Miriam Odemba ameanzisha taasisi yake ya kujitegemea inayoitwa ‘Run with Odemba’.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.