Mke Wangu Nimemvisha Pete Huu Mwaka Wa 3 Hakuna Harusi – Peter Msechu

Mwanamuziki wa Bongo fleva Peter Msechu aliyetamba na ngoma zake kama Nyota na nyinginezo amefunguka na kueleza kuwa mwanamke anayeishi naye na aliyezaa naye mtoto hajafunga naye ndoa mpaka leo.

Msechu alifunguka na kuongelea hayo baada ya harusi ya staa Shile na mume wake Uchebe kuzizima na kuvutia wengi ikiwemo mastaa wenyewe. Ndoa hiyo iliyokuwa imehudhuriwa na mastaa kibao ilifana kupita kiasi huku mastaa hao wakiacha rekodi baada ya kumwaga mizawadi kibao kwa maharusi.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Millard Ayo TV Peter Msechu amefunguka Mengi kuhusu kuvutiwa na harusi hiyo na mipango yakea ya kufanya harusi yake mwenyewe:

kwanza ningependa kumpongeza Shilole na bwana Uchebe kwa kufikia maamuzi makubwa ya namna hiyo unajua sisi wasanii ambao tumeshakaa na familia zetu kwa muda mrefu kufanikisha hatua hiyo bado kwa kweli wanahitaji kupongzwa mimi binafsi nilishataka kufunga harusi muda mrefu sana lakini kila nikitaka kuanza kufunga harusi bikifikiria kianza vikao haaa naachia kati yaani ninavyokwaambia mwanamke wangu nimemvisha Pete huunimwaka wa tatu kila nikitaka ya mipango nikiwaza hela ya harusi nakumbuka ndani unga Hamna”.

Baada ya ndoa ya Shilole na Uchene mastaa kibao wamesema na wenyewe wako nyuma wanafuatia mastaa kama Dogo Janja na Irene Uwoya.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.