Mrembo Kim Nana Adai Amber Lulu na Gigy Maney Sio Level Zake

Video Queen anayekuja kwa kiasi ya ajabu Kwenye tasnia Lilian Paul Kessy maarufu kama Kima Nana amewaponda vibaya mno wasanii Amber Lulu na Gigi Money huku akidai hawafai kuwa mavideo vixen.

Kim Nana alijizolea umaarufu baada ya kuonekana kwenye video za wanamuziki kama Beka Flavor ameibuka na kudai mavideo Queen hao ambao wameongia Kwenye Bongo fleva hawakuwa level zake.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Global Publishers, amefunguka na kudai ni bora wadada hao walivyoingia Kwenye muziki kwani hawakuwa na mvuto wa kuwa wauza sura wa Kwenye video:

Amber Lulu na Gigy Money hawanivutii kabisa na hawana mvuto wa kuwa ma-video queen. Bora ‘wa-stick’ hukohuko kwenye muziki walikokimbilia”.

Lakini pia mrembo huyo alijitamba ni bora kuliko mavideo Queen wote kwa Bongo kwa sababu ana muonekano wa kuwa hivyo tofauti na ilivyokuwa kwa Gigy Money na Amber Lulu.

Amber Lulu

Kim Nana alipoulizwa kuhusu tuhuma za mavideo Queen wengi Bongo kutembea na wasanii mbali mbali ili wapate umaarufu alikataa na kudai yeye yupo kikazi zaidi hana time hiyo:

Mimi ninajiheshimu, nikiitwa na mwanamuziki kuhusu kazi, tunafanya halafu basi. Tutaendelea kuwasiliana kwenye mambo mengine, lakini siyo mapenzi. Sijawahi kutoka kimapenzi na staa yeyote Bongo na sitarajii hilo kwa sababu kuwa na uhusiano na mastaa kuna-umiza kichwa. Wengi hawa-jatulia“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.