Msemaji wa Magereza Akanusha Uhuru wa Lulu Michael
Huku taarifa za habari za furaha zikianza kusambaa katika vyombo mbalimbali kuhusu msanii Lulu Michael kuwa huru baada ya kusemekana kuwa kifungo chake kuisha lakinimsemaji wa magereza amekanusha taarifa hizo na kusema kuwa lulu bado ni mfungwa kama wafungwa wengine na kifungo chake kitakapoisha atakuwa hurulakini si sasa.
Msemaji huyo anasema kuwa kwa kawaid ahaweiz kuwa huru kama hajafata utaratibu wa magerezawa kuachi wa huu hata kama hakuwa akiishi gerezani kwa kipindi cha muda mrefu kutokana na kutumikia kifungo chake cha nje.
Msemaji wa magereza anayasema hayo baada ya kuona kuwa taarifa za kuwa huru kwa mwanadada huyo zimesambaa sana katika mitandao ya kijamii, “taratibu nadhani anazifahamu kwa sababu lazima kuna utaratibu wa kufuatwa kabla ya kuwa huru, na hata kama yuko kifungo cha jje kuna utaratibu anafuata pia kama wafungwa wengine tu hata kama ni mtu maarufu , kile ambacho lulu anafanyiwa ni kama anaweza kufanyiwa mfungwa mwingine yoyote yule...”
Msemaji huyo anasema kuwa kama ilivyo kwa wafungwa wengine kuwa hawakutangazwa kipindi anawekwa ndani na ndivyo itakavyo kuwa akiwa anatoka, na hata kama alikuwa na kifungo cha nje haimaanishai kuwa anatakiwa kuondokea huko huko uraiani bali anapaswa kurudi magereza na kufuata taratibu za kumaliza kifungo na ndipo atakapokuwa hur na maisha yake ya nje..