Mtangazaji Wa Burundi Aongelea Utapeli wa PCK , Athibitisha kuwa PCK ndio Mvujisha video Za Wema
Moja ya watangazaji nchini burudni katika tv na radio ya rhema Fm amefunguka na kutoa ushaidi wa kuwahi kutapeliwa na mwanaume aliyewahi kusemekana kuwa ni mume mtarajiwa wa wema sepetu.
Mtangazaji huyo aliejulikana kwa jina la aveick anasema kuwa hata yeye aliwahi kuwa rafiki na PCK Kwa muda wa miaka miwili na walipanga kufanya kazi ya muziki pamoja kwa sababu PCK alimwambia kuwa yeye ni msanii na anaitaji promo nchi Burundi.
Aveick anasema kuwa baada ya muda alimuamini mwanaume huyo na hata kumtumia pesa kwa ajili ya kumnunulia simu nchini tanzania , simu ambayo aliipenda na PCK alimwambiakuwa na yeye anayo.
Hata hivyo mtangazaji huyo anasema kuwa PCK amekuwa tapeli kwa muda mrefu na wala sio mara ya kwanza kutapeli wanawake.
Aveick anasema kuwa hata picha na video za wema yeye ndio aliekuwa akiposti na kuzituma mitandaoni na kwa naman moja amna nyingine wamekuwa wakimshuku kuwa mwanaume huyo kuna nguvu ya ziada amekuwa akitumia kuwarubuni wadada.