“Mume Wangu Angenishangaa Kama Nisingemsaidia Ruge”- Zamaradi

Mtangazaji na mdau mkubwa wa Bongo movie Zamaradi Mketema amefunguka na kuweka wazi sababu ya kuwa mstari wa mbele kuhamasisha michango kwa ajili ya matibabu ya baba Watoto Wake Ruge Mutahaba.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Zamaradi alisema kuwa angeonekana mtu wa ajabu na watu wangejiuliza endapo na yeye angekuwa nyuma kutohamasisha watu kuchangia matibabu ya Ruge ambaye pia ni baba wa watoto wake wawili.

download latest music    

Unajua watu wangekuwa kwenye mshangao endapo nisingefanya kitendo cha uungwana cha kuamua na mimi kuchangisha. Hata mume wangu angenishangaa, lakini pia ugonjwa siyo kitu cha kufanya mashindano hata kidogo maana yeyote anaweza kuumwa“.

Watoto wangu wanampenda baba yao na wanampenda baba anayewalea hivi sasa, lakini mimi kutoonesha kuguswa katika hili, hata watoto wangu wangenishangaa sana. Unajua suala la mgonjwa linamgusa kila mtu”.

Ruge alianza kuchangiwa fedha za matibabu mwanzoni mwa wiki hii baada ya familia yake kuomba kusaidiwa katika kipindi hiki ambacho jamaa huyo anaendelea na matibabu ya matatizo ya figo nchini Afrika Kusini.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.