Mwana Fa Ajihakikishia Kupata Kazi Sehemu Yoyote.

Msanii wa muziki mkongwe nchini Mwana Fa , amefunguka na kusema kuwa kuna kipindi alishawahi kupata changamoto sana katika kazi yake ya muziki na kumfanya akate tamaa na kutaka kuacha muziki ili aende kuajiriwa sehmu nyingine.

Mwana Fa anasema kuwa pamoja na kwamba alikuatana na changamoto za kumkatisha tamaa lakini aliona sio vyema kuacha kazi ya muziki na kwenda kuajiriwa ingawa akitaka kwenda kuajiriwa anaweza kuapata kazi muda wowote.

download latest music    

mimi kuna kipindi nilikuwa na wakati mgumu na nikafikiria kuwa muziki wenyewe nataka kuachana nao nifanye shughuli nyingine  na bahati nzuri mimi nina backup kabisa na kazi zangu.

ningewez akutoa vyeti vyang na  na nikaendelea na shughuli zingine fresh tu lakini mimi nina back up nzuri na pia nina cinnections nzuri tu , nikitaka kuanza kazi ninaaanza tu hata wiki ijayo tu,kwenda kazini saa mbili mpaka saa 11, yaani hilo sio swala la kujiuliza kabisa.

Mwana Fa anasema kuwa katika kila kazi hakuna sehemu yenye urahisi wa kila kitu kwaio hata kama angeacha kazi ya uziki na kwenda kuajiriwa hasingekuta kuwa huko ndio kuna mambo rahisi sana,maana hakuna sehem iliyotambarare tu , hivyo kitu cha kufanya ni kujikaza na kufanya kazi kwa moya na kujituma bila kukata tamaa na hili amewashauri hata wasanii wengine.

Mwana Fa ni moja kati ya wasanii wachache wasomi wenye kujivunia muziki wao pamoja na elimu kubwa walionayo, hivyo ukiachana na kazi ya muziki lakini pia ni msanii msomi mwenye uwezo wa kuajiriwa kokote kulingana na elimu yake.

Wapo baadhi ya wasanii wamekuwa wakitokomea kusiko julikana na kuacha kazi ya muziki kwa sababu ya mambo magumu wanayokuwa wanakutana nayo katika tasnia.Wengi wanakata tamaa na kuishia njiani.Wapo wanaoinuka kwa kuinuliwa na wapo wanaorudi nyuma na kukumbuka mafanikio yao na wanajipa matumaini lakini pia wapo wanaokata tamaa kabisa na kufa kimuziki moja kwa moja.Mwana Fa anawashauri na kuwatia moyo wasanii kuacha kukata tamaa.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.