Nai Atishia Kuwavua Nguo Mastaa

Video vixen na make up artist maarufu Bongo kwa sasa Nai amefunguka na kudai siku si nyingi atakuja kuwavua nguo wasanii wakubwa ambao wamegoma kumlipa.

Nai ambaye kwa sasa ana saluni yake kufanyia make up (Nai Beauty) amekuwa akifanya kazi na wasanii mbali mbali wa Bongo fleva na Bongo Movie lakini hawamlipi kwa huduma wanayopata.

download latest music    

Kwenye mahojiano na kipindi cha Enews cha EATV, Nai amedai endapo hawatamlipa basi kinachofuata ni kuwavua nguo kwa kuyaanika majina yao na baada ya hapo ni kuwakusanya man kuwapeleka polisi.

Habari hii iwafikie mastaa wote ambao hawajanilipa kwamba ninawapa wiki kadhaa ambaye hatakuwa amenilipa atakutana na deni  lake Enews yaani nitamuanika kuanzia juu mpaka chini”.

Lakini pia Nai ametishia kuwachukulia hatua za kisheria Mastaa hao endapo kuwadhalilisha haitawasukuma kumlipa:

Wapi wasanii nimewaweka Kwenye mabano kama  watatu hivi na ni wasanii wakubwa tu nasema hivi nitawadhalilisha kwa kuwaposti Kwenye mitandao ya kijamii na nikimaliza nawapeleka polisi kwa sababu sio vizuri mimi ni msichana mdogo nafanya kazi nahustle kutafuta alafu tunafanyiana hivi Jamani?”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.