Nandy Azima Tetesi Za Kuwa Mjamzito

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva Faustina Charles maarufu kama Nandy amefunguka na kukataa kata kata tetesi zilizombaa Kwenye mitandao ya kijamii kuwa hivi sasa ni mjamzito.

Nandy ambaye hivi sasa anafanya vyema kabisa na ngoma yake ya ‘Aibu’ amekataa tetesi za kuwa hivi sasa amejazwa kibendi na Kigogo mmoja na kudai ni uzushi tu.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Nandy alisema watu huwa wanaamua tu kuzusha mambo yasiyokuwa na ukweli wowote ule ndani yake, ili mradi tu wafurahishe mioyo yao kitu ambacho kinaumiza.

Hizo tetesi zinazosambaa mitandaoni kwamba nina mimba siyo za kweli, ila naona watu wameamua tu kuzizusha ili wafurahishe mioyo yao, sina mimba jamani naomba waniache“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.