Nawapenda Wanawake Waliokaza,Sio Wema -Rado

Msanii wa maigizo nchi ambae pia alishawahi kujaribu upande wa  muziki na akafanya vizuri anaejulikana kama Rado, amefunguka na kusema sifa za mwanamke anaempenda lakini amekanusha kabisa kuwa yeye hawezi kutembea na mwanamke anaetoka Bongo Movie au Bongo Fleva.Msanii huyo ambae alikuwa akiongea na waandishi wa habari na kuulizwa kuhusu kazi yake iliyo toka kipindi cha nyuma kidogo , filamu ambayo alicheza na Tanzanian Sweetheart Wema Sepetu  iliyojulikana kwa jina la “Madame’ ambayo pia ilizua maneno na  tetesi za msanii huyo wa kiume kutoka kimapenzi na Wema Sepetu, Rado alifunguka na kusema hawezi kutembea na Wema hata kidogo.

‘Sijawahi kumpenda msanii yeyote wa Bongo Movies au wa Bongo Fleva wa kike na siajwahi tu kuvutiwa nao  hata kidogo, sijawahi  kuvutiwa na Madame Wema Sepetu kwa sababu naona yupo nje ya wanawake ninao wapenda” alifunguka rado, lakini pia msanii huyo wa  alitoa sababu za yeye kutokuvutiwa kimapenzi na msanii wa kike akiwemo madame Wema Sepetu au wanawake wote kutoka Bongo Movie na Bongo Fleva na kusema kuwa “unajua mimi ni mchanganyiko wa Usukuma na Unyakyusa, kwaiyo wanawake wa kudeka  muda wote siwapendi, napenda  wanawake fulani hivi waliokaza” ameongezea Rado

download latest music    

Akielezea experience aliyoipata kutoka kwa Madame Wema wakiwa katika kuigiza filamu ya ‘madame’ , Rado anasema kuwa Wema Sepetu anaonekana mwanamke wa kudeka sana kwaiyo mtu kama huyo hawatawezana kwabisa,” kwa jinsi alivyokuwa mlegevu Madame, sina hata uhakika  hata kama anaweza kufua , kutokana na kudeka kwake” anaendelea Rado

kwa upande wa Bongo Movies, Rado anasema kuwa kwa sasa tasnia  ya filamu inaendelea kufanya vizuri kutokana na jitihada zinazofanyika ili kulinda vipaji vya wasanii ambapo kumekuwa  na kampeni mbalimbali ikiwemo ile ya kusimamisha uuzaji wa filamu fake mitaani na anasema kwa sasa vilio wa wasanii wa filani  vinaelekea kuisha na wataanza kuona maslahi ya kazi wanazofanya na kuna baadhi ya makampuni yamejitolea ilii kusimamia kazi za wasanii katika uuzaji.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.