NAY Wa Mitego Afunguka Kuhusu Nini.

Msanii wa bongo fleva nchini Ney wa Mitego amefunguka na kutilia mkazo swala la watu kusambaza maneno kuwa yeye na msanii mwenzake anaekuja vizuri katika swala la muziki, nini wamekuwa na  mahusiano ya mapenzi kwa muda mrefu,ney wa mitego anasema kuwa watu wanaosambaza taarifa hizo hazina ukweli wowote lakini anashindwa kuendelea kuongea kwa sababu watu walishaweka maneno midomoni tayari.

Siku za nyuma , Ney wa Mitego na Nini walisemekana kuwa katika mahusiano ya kimapenzi ya muda mrefu na kusemekana kuwa sababu kubwa ya meneja wa Nini (Daxo Chali ) kuvunja mkataba nao ni kwa sababu Ney wa Mitego amekuwa akim-control na kumfanya mwanadada huyo kushindwa kufanya kazi  vizuri .

download latest music    

Ney wa Mitego anasema kuwa tatizo la mashabiki wengi hata wakiambiwa nini wanakuwa tayari wameshajiwekea maneno yao midomoni kwaio hakuna haja ya kusema neno lolote la kumfanya mtu uyo aamini.

Unajua ukiwaambia watu kuwa ni marafiki tu hawakuelewi,ukiwaambia kuwa unafanya nae kazi wala hawatakuelewi  basi na mimi nafikiri kwa sasa imetosha , jibu ninalo moyoni mwangu. -Alisema Ney Wa Mitego.

wawili hao hivi karibuni walitoa wimbo mpya unaoitwa Niwe Dawa,ambapo baada ya wimbo huo watu wengi walidhani kuwa nini kwa sasa atakuwa chini ya lebel ya ney wa mitego lakini nini mwenyewe alikanusha habari hizo na kusema kuwa kwa sasa hana menejiment yoyote

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.