Nay Wa Mitego: Nimeshazoea Kuishi Maisha ya Kimaskini

Mwanamuziki Wa Bongo fleva Ney Wa Mitego amefunguka kuwa ameshazoea kuishi maisha ya kimaskini kama Mtanzania yoyote yule mwenye kipato cha hali ya chini.

Ney alifunguka hayo baada ya habari kuenea kuwa ameuza nagari yake yote na anaonekana mtaani akitembea kwa miguu na kupanda bajaji, huku watu wengi wakidai kuwa amefulia ndio maana ameamua kuuza magari yake yote.

download latest music    

Katika mahojiano aliyoyafanya na kituo cha televisheni cha East Africa Ney alimwambia mwandishi anatamani Watanzania waache apumue na waache kumsakama kuwa amefulia kwani ndio maisha aliyoyachagua mwenyewe.

Ney alifunguka;

“Jamani niacheni nipunue haya ndio maisha yangu niliyoyachagua, kupanda daladala ama Bajaji ni sehemu ya maisha yangu, Mimi nimetokea mtaani siwezi kuishi bila kuheshimu mitaa, jata marafiki zangu ukiwaangalia ni Wa kawaida Sana, kwaiyo kutembea kwa miguu isiwe tabu, halafu Kama hujagundua mimi napenda maisha ya kawaida, siishi kistaa Kama wengine, na pia nikiishi hivi nakuwa huru zaidi”.

Ney Wa mitego amwyaongea hayo baada ya kuzidi kuandamwa na maneno ya watu wanaodai ameishiwa hana kitu baaada ya kuonekana mitaani akipanda Bajaji na kusemekana ameuza magari yake yote aliyokuwa anamiliki.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.