“Nimepigwa Kama Mtoto na Uchebe Kisa Soudy Brown”- Shilole

Msanii wa Bongo fleva Shilole amefunguka na kuelezea kichapo kizito alichotembezewa na mumewe Uchebe ambapo amedai kisa na mkasa ni yeye kucheza mziki na Soudy Brown kwenye sherehe.

Siku ya jana kwenye kipindi cha XXL, Soudy Brown alifunguka kuwa alipokea taarifa kuwa Shilole alipokea kichapo kizito kutoka kwa mumewe Uchebe baada ya kurudi nyumbani usiku wa manane akitokea kwenye party Tabata.

download latest music    

Kupitia kwenye ‘You Heard’ Alitafutwa na kuulizwa kuhusu tetesi za kupokea kichapo hicho usiku usiku Shilole alikiri na kufunguka haya:

Tena Soudy niache kabisa wewe ndio umefanya mpaka mimi nagombana na Mume wangu eti Uchebe ana sema wewe bwana angu kweli? Umeshawahi kunitongoza wewe? Eti kisa siku ile kule Tabata tulivyokuwa tumekaa meza moja eti kakasirika, tulivyokuwa tunacheza mziki kwaiyo ina maana mimi nisicheze na mashabiki eti! MImi sitaki kuhusu kuongea mambo mengi nikaonekana mkorofi wa ajabu”.

 Lakini pia Shilole alikiri kupigwa kama mtoto na Uchebe kiasi kuwa walifunga mtaa hadi kupelekea Shilole kwenda kulala kwa marafiki zake:

Yaani Uchebe amenipiga kama mtoto mdogo lakini haina noma mimi mwanamke na dunia nzima inajua mimi mwanamke kuna mambo mimi nitakuja kusema mazito alafu ndo nitakapodai Talaka yangu”.

Baada ya sakata hilo Shilole alienda kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuweka ujumbe huu:

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.