“Nipo Tayari Kuzaa Mtoto Mwingine”- Aikah

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka kundi la Navykenzo, Aikah Navykenzo amefunguka kuhusu mipango yake ya kuzaa mtoto mwingine hivi karibuni.

Aikah ambaye alijifungua mtoto wake wa kwanza miezi miwili iliyopita na  mpenzi wake wa miaka mingi Nahreel amekiri kuwa ana mpango wa ‘kutengeneza’ wengine zaidi ya huyu aliyenaye sasa.

download latest music    
Gold Navykenzo

Tarehe 9 December mwaka jana Aikah alijifungua mtoto wake wa kwanza waliyemuita Gold Navykenzo lakini siku ya jana miezi miwili baadae Aikah kashasema anataka kuzaa mtoto mwingine.

Gold akiwa na Baba yake Nahreel

Siku ya jana ilikuwa ni sherehe ya kumbukumbu ya siku ya kuzaa kwa Aikah na kupitia ukurasa wake wa Instagram Aikah alifunguka kuhusiana na mipango yake ya kuzaaa mtoto mwingine ambapo aliandika maneno haya machache:

Najisikia msichana mbichi zaidi na nipo huru zaidi kwenye mwili wangu mwenyewe niko tayari kufanya kazi kwa nguvu zaidi, kutengeneza muziki mzuri, kusafiri na kuzunguka duniani na hata nipo tayari kwa ajili ya kuzaa watoto wengine… Nashukuru kwa kunitakieni heri katika siku yangu ya kuzaliwa nawapenda wote”.

Tangu ajifungue Aikah na Nahreel wamerudi kwenye jitihada zao za kutengeneza mziki kwani ni wiki chache zilizopita walienda nchini South Africa kurekodi video ya nyimbo yao mpya lakini inasemekana kuwa walisafiri na mtoto wao Gold.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.