Ommy Dimpozi aonekana kituo cha polisi cha kati

Msanii wa bongo fleva Ommy Dimpozi anaetamba na nyimbo zake kama kajiandae aliomshirikisha alikiba lakini pia ametoa wimbo mpya hivi karibuni unaojulikana kwa jina la ‘cheche’  ameonekana maaeneo ya polisi kituo cha kati alipokwenda kwenye mahojiano kwa takribani zaidi ya saa tano.

Ommy Dimpozi jana septemba 13 alionekana kituo cha polisi majira ya saa tano asubuhi akiingia kituoni hapo huku akiwa ameongozana na watu wawili  katika gari aliyokuja nayo, hata hivyo kwa zaidi ya masaa matano Ommy Dimpozi hakuonekana kutoka mpaka mida ya saa 10:30 jioni , kwa mujibu wa waandishi wa habari ambao walikuwa kituoni hapo kufatilia press conference ya  kamanda wa polisi Mambosasa walisema walimuona Ommy Dimpoz akiingia kituoni hapo.

download latest music    

Hata hivyo jitihada zilizofanywa na waandishi wa habari wa Ayo tv za kumuhoji msanii huyo kuhusu uwepo wake kituoni hapo kwa zaidi ya saa tano , Ommy Dimpoz alijibu kuwa “ni mahojiano ya kawaida tu..tutaongea ila kwa sasaivi siruhusiwi kusema chochote” alisema Ommy Dimpozi  na kuondoka.

Kwa habari ambazo hazijathibitishwa ni kwamba inawezekana sababu ya Ommy kuwepo kituoni hapo kuhojiwa ni kutokana na post yake aliyoipost siku zilizopita hivi karibuni inayomuhusu mama Diamond, na kwa kumbukumbu ni kwamba wasanii hawa wawili walikuwa katika vita ya kimtandao ambayo ilifikia hadi kumhusisha mama mzazi wa Diamond., na bado haijafahamika bado  ni nani hasa aliyepleka kesi hiyo kituoni hapo kati ya familia ya Diamond au Diamond mwenyewe, lakini ilhali amehaidi kuliongelea swala ilo tunasubiri Ommy afunguke zaidi.

Hata hivyo, baada ya press conference , mkuu wa kituo hakuongelea chochote kuhusu msanii huyo kuwepo kituoni hapo.

Ni week chache zimepita tangu kuwepo kwa mfarakano wa team kiba na team diamond ambapo Ommy ni supporter mkubwa wa team kila ilhali katika kumbukumbu za awali  ommy dimpozi alikuwa mtu wa karibu kabisa sana wa  diamond platnumz na hakuna aliyewahi kufikiria kuwa kutakuwa na bifu zito kati ya wawili hao.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.