Picha za Alikiba na Shabiki Zilizozua Utata Mtandaoni

Mwanamuziki Alikiba alizua utata baada ya picha zake na shabiki wake kuvuja mtandaoni. Alikiba alikuwepo jijini Mwanza kwa ajili ya tamasha la Fiesta lililofanyika jana lakini picha alizopiga na msichana ambaye hakutambulika mara moja zilileta utata kidogo miongoni mwa watu hasa sababu ya pozi tata za picha hizo. Huku kila mtu akisema lake mtandaoni hakuna mtu aliyemtambua mwanadada yule.

Hizi ni baadhi ya picha hizo zilizozua utata:

download latest music    
1.
2.
3.

Picha hizo zilizomuonyesha katika mapozi mbalimbali na mwanadada huyo ziliamsha minong’ono baada ya mashabiki kuanza kudhani kuwa ni mpenzi wake, lakini baada ya muda chanzo cha karibu cha Alikiba kiliachia picha huku kikisisitiza kuwa Ali hana uhusiano wowote na mdada yule zaidi ya urafiki wa kawaida tu.

Upande wa Alikiba waliachia picha hizi pia;

1.
2.

Msemaji wa Alikiba alisistiza kuwa hizo picha zote zilipigwa kwa wakati mmoja akijibu maswali ya watu kuwa ni kwanini alipiga picha na msichana chumbani, “Hizo picha zote zilikuwa ni Alikiba akipiga na mashabiki zake waliomfata kuomba picha za pamoja”. Ali kiba alimaliza kiu ya wakazi wa Mwanza kwa kupiga bonge la shoo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.