Q-Chillah Atoa Shukrani Zake kwa Mh.Rais
Msanii mkongw wa muziki wa bongo fleva q-chillah amefunguka na kusema kuwa moja ya watu anaowashukuru sana mabao hawakutaka yeye aachane na muziki ni mh rais ambae aliwatuma watu na kwenda kuongea nae ili asiweze kuacha muziki.
Chillah anasema kuwa hapo ndipo alipomini kuwa muziki wake una mchango mkubwa sana na mpaka kufikia hatua ya mh raisi kutuma wajumbe kwenda kumuomba yeye hasiache muziki kwake ni jambo kubwa sana.
Chillah ambae alikuwa ametangaza kuachana na muziki kutokana na athari kubwa alizowahi kuzipata za kutumia madawa ya kulevya kutokana na muziki huo huo anasema kuwa kwake yeye hiyo ilikuwa ni heshima kubwa sana.
Baada ya interview nilipata meseji na simu nyingi sana kutoka kwa watu mbalimbali,na nilifarijika zaidi nilipoona Mh. Rais ametuwa watu wake waje kuongea na mimi nisache muziki taifa bado linanihtaji.